Sunday, October 15, 2006

WAHAKA

[1]
Rabbi Mola Mswifika,
Muumba na kuumbuwa
swifazo mekamilika,
hakuna lilopunguwa
Rabbi nondosha wahaka
mahaba yataniuwa,

[2]
Ya Ilahi Mtajika
nakuomba we Moliwa
Wahadahu Ia shirika
nguvu zisomithiliwa
Rabbi nondosha wahaka
mahaba yataniuwa,

[3]
Enzi ni yako hakika
ni yupi tena wa kuwwa?
Bwana ulotakasika
na usiye shabihika.
Rabbi nondosha wahaka
mahaba yataniuwa.

[4]
Aridhi umetandika
mbingu na mwezi na juwa
na nyota zilopambika
usiku unapokuwa.
Rabbi nondosha wahaka
mahaba yataniuwa.

[5]
Usiye na ushirika
kutaka kushauriwa
waona usooneka
tangu isotanguliwa.
Rabbi nondosha wahaka
mahaba yataniuwa.

No comments: