Sunday, October 15, 2006

NYONDA

[1]
Laaziza, muhibu liakirami
Pulikiza, nikupe wangu usemi
Menikaza, sipati kunena yomi.
[2]
Wangu moyo, una jambo uupete
Wayowayo, liniveme kana Pete
Zangu mbio, nataraji tuwe sote
[3]
Si moyoni, jaraha kulla mahali
Na matoni, sipati lepe silali
Masikini, napenda kitu ki ghali
[4]
U kizani, moyo umefitamana
Na imani, viumbe huoneana
Swamahani, sinifanyiye khiyana
[5]
Hikuwaza, iwapo nala huata
Miujiza, muda hilala huota
Niuguza, maradhi yalonipata
[6]
Yomi bui, mwenziyo nimedangana
Hunijui, moyoni ninavyoona
Sinwi shai, nisikutaje kwa jina
[7]
Yomi toba, mwenziyo ni taabani
Kwa mahaba, yalonivaa moyoni
Hunikaba, wala utungu sioni.
From Malenga wa Mvita by Ahmad Nassir

No comments: