[1]
Twakuomba mtukufu.
Asokijana na kufu.
Mola wetu maarufu.
AlIahu alo karima.
[2]
Mikono tumeinua.
Mola wetu watujuwa,
Takabali yetu duwa.
Utupe lililo nawema.
[3]
Mola machozi yatoka.
Hakika ya bubujika,
Tumetubu kwa hakika.
Waja wako tumekoma.
[4]
Rabbi sisi waja wako.
Twatubu twa rudi kwako.
Tutini ya twaa yako.
Tukubaile karima.
[5]
Ya Rabbi tupe Ilimu.
Tupe na njema Fahamu.
Ya kutambua vigumu.
Vya dini yako Karima.
[6]
Utupe matunda yake,
Tuisome tusichoke.
Mola ilimu iweke.
Moyoni mahala pema
[7]
Rabbi ijapo hukumu.
Isiwe kwetu ni ngumu,
Tusiweze kudhulumu.
Tukuche wewe Karima.
[8]
Turuzuku nyingi hima
Isiokuwa na kukoma.
Utupe na kulla jema.
Duniani na kiama.
[9]
Tupe Riziki halali.
iso na uthakili.
Utupe na njema hali
Duniyani na kiyama.
[10]
Tuondoshee laudhiya.
Lilo na kulla baliya,
Utupe liso udhiya.
La-dini yako karima.
[11]
Utupe na kupendana.
Sisi na wetu vijana,
Mapenzi yaso khiyana.
Ya dini yako karima.
[12]
Utupe njema fasaha
iso kuwa najaraha.
Utupe nyingi furaha,
Duniani na kiyama.
[13]
Tutunze mijini mwetu.
Tukidhie deni zetu.
Kabla ya kuja kwetu,
Mjumbe wa mauti mwema.
[14]
Sizi vunde zetu hima,
Tuawini wima wima.
Utujaze yako mema.
Duniani na Kiyama.
[15]
Tubarikie Jalili.
Umriwetu twawili.
Sote na kulia adili.
Afunzae kula jema.
[16]
Kulla ajae na shari.
Waijuwa yake siri
ivunde yake dhamiri.
Asiweze kusimama.
[17]
Rabbi swala na salamu.
Umfikilie hashimu
Na sahaba ze kiramu
Na alo kulla mwema
[18]
Amina Rabbi Amina
Amina Rabbi Amina
Amina Rabbi Amina.
Tukubalie Karima.
Twakuomba mtukufu.
Asokijana na kufu.
Mola wetu maarufu.
AlIahu alo karima.
[2]
Mikono tumeinua.
Mola wetu watujuwa,
Takabali yetu duwa.
Utupe lililo nawema.
[3]
Mola machozi yatoka.
Hakika ya bubujika,
Tumetubu kwa hakika.
Waja wako tumekoma.
[4]
Rabbi sisi waja wako.
Twatubu twa rudi kwako.
Tutini ya twaa yako.
Tukubaile karima.
[5]
Ya Rabbi tupe Ilimu.
Tupe na njema Fahamu.
Ya kutambua vigumu.
Vya dini yako Karima.
[6]
Utupe matunda yake,
Tuisome tusichoke.
Mola ilimu iweke.
Moyoni mahala pema
[7]
Rabbi ijapo hukumu.
Isiwe kwetu ni ngumu,
Tusiweze kudhulumu.
Tukuche wewe Karima.
[8]
Turuzuku nyingi hima
Isiokuwa na kukoma.
Utupe na kulla jema.
Duniani na kiama.
[9]
Tupe Riziki halali.
iso na uthakili.
Utupe na njema hali
Duniyani na kiyama.
[10]
Tuondoshee laudhiya.
Lilo na kulla baliya,
Utupe liso udhiya.
La-dini yako karima.
[11]
Utupe na kupendana.
Sisi na wetu vijana,
Mapenzi yaso khiyana.
Ya dini yako karima.
[12]
Utupe njema fasaha
iso kuwa najaraha.
Utupe nyingi furaha,
Duniani na kiyama.
[13]
Tutunze mijini mwetu.
Tukidhie deni zetu.
Kabla ya kuja kwetu,
Mjumbe wa mauti mwema.
[14]
Sizi vunde zetu hima,
Tuawini wima wima.
Utujaze yako mema.
Duniani na Kiyama.
[15]
Tubarikie Jalili.
Umriwetu twawili.
Sote na kulia adili.
Afunzae kula jema.
[16]
Kulla ajae na shari.
Waijuwa yake siri
ivunde yake dhamiri.
Asiweze kusimama.
[17]
Rabbi swala na salamu.
Umfikilie hashimu
Na sahaba ze kiramu
Na alo kulla mwema
[18]
Amina Rabbi Amina
Amina Rabbi Amina
Amina Rabbi Amina.
Tukubalie Karima.
2 comments:
Fantastic, Mungu akujazi kheri. Please hebu angalia hiyo namba 4 iko na typo error.
Iko sawa, Tutini means tuko chini :)
Post a Comment